Klabu ya Real Madrid itashuka uwanjani kwa miezi mitatu
bila ya kuwa na kiungo wake mkongwe, Xabi Alonso ambaye amevunjika mfupa katika
mguu wake wa kulia.
Taarifa iliyotolewa na klabu hiyo, imesema kiungo
huyo baada ya kufanyiwa uchunguzi amegundulika amevunjika mfupa wa juu wa juu
wa mguu wake wa kulia hivyo atakuwa nje ya uwanjani kwa miezi mitatu.
Nyota huyo ana uwiano wa kucheza michezo 40 katika
mashindano yote inayoshiriki Madrid kwa msimu, aliumia katika mchezo wa
ufunguzi wa Ligi ya Hispania, La Liga dhidi ya Real Betis ambao walishinda
mabao 2-1 mwishoni mwa wiki iliyopita.
Kwa mujibu wa taarifa hiyo Alonso anatarajiwa kurudi
uwanjani mwishoni mwa mwezi Novemba au mwanzoni mwa Desemba kama atafanyiwa
uchunguzi na kuhakikisha kuwa mguu wake umepona vizuri.
0 comments