PAMOJA na aliyekuwa kipa wa Simba, Juma Kaseja
kutokuwa na timu baada ya kuachwa na timu yake ya zamani lakini Kocha Mkuu wa
Taifa Stars, Kim Poulsen amemjuisha katika kikosi chake kitakachoivaa Gambia
katika mchezo wa mchujo ya Kombe la Dunia utakaochezwa Septemba 7 mwaka huu
nchini humo.
Kaseja alitemwa mwishoni mwa msimu ulioipita kwa
madai ya kushuka kwa viwango ameitwa katika timu ya wachezaji 24 wanaotarajiwa
kuingia kambini Agosti 29 mwaka huu kabla ya saa 1 kamili usiku. Kambi ya Taifa
Stars inayodhaminiwa na Kilimanjaro Premium Lager itakuwa kwenye hoteli ya
Accommondia jijini Dar es Salaam.
Mbali na Kaseja wachezajki wengine walioitwa katika
kikosi hicho ni pamoja na makipa Mwadini Ali (Azam), Ally Mustafa (Yanga) na
Aishi Manula (Azam). Mabeki ni Aggrey Morris (Azam), Kelvin Yondani (Yanga),
Shomari Kapombe (Simba), Nadir Haroub (Yanga), Erasto Nyoni (Azam), Vincent
Barnabas (Mtibwa Sugar) na David Luhende (Yanga).
Viungo Khamis Mcha (Azam), Salum Abubakar (Azam),
Said Dilunga (Ruvu Shooting), Frank Domayo (Yanga), Athuman Idd (Yanga), Haruna
Chanongo (Simba), Amir Kiemba (Simba), Mrisho Ngasa (Yanga), Simon Msuva
(Yanga), John Boko (Azam), Thomas Ulimwengu (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi
ya Congo), Mbwana Samata (TP Mazembe, Jamhuri ya Kidemokrasi ya Congo) na Juma
Liuzio (Mtibwa Sugar).
0 comments