Saa nne usiku leo dunia itasimama kupisha mchezo wa
kukata na shoka kati ya Chelsea itakuvaana na Manchester United kwenye Uwanja wan
Old Trafford.
Mchezo huo leo umebeba vitu vingi ambavyo vimeufanya
uonekane kuwa na mvuto wa aina yake na kuvuta hisia za mashabiki lukuki wa soka
duniani kote.
Kivutio cha kwanza katika mchezo huo ni pale timu
hizo ziotakapovaana zikiwa na makocha wawili wapya ambao watakuwa katika benchi
kwa mara ya kwanza miamba hiyo itakapokutana.
Jose Mourinho atakuwa anaiongoza kwa mara ya pili
ataivaa Manchester United wakati kwa upande wa David Moyes atakuwa kwenye
benchi la Man Utd akivaana na Chelsea.
Utamu mwingine katika mchezo huo utakuwa pale
mshambuliaji wa Manchester United, wayne Rooney anayewania kwa hali na mali na
Mourinho, ataanza katika kikosi cha kwanza cha United.
Mashabiki wa soka duniani kote wana kiu ya kujua
kama nyota huyo ambaye Mourinho anamsubiri mara baada ya kumalizika kwa mchezo
huo atafanya nini atakapokuwa uwanjani leo?
Leo hakuna mtu atakayetumwa dukani wakati miamba
hiyo iutakapokuwa uwanjani kusaka pointi tatu muhimu katika msimamo wa Ligi Kuu
ya England.
DONDOO MUHIMU
Timu: Manchester United v Chelsea
Uwanja: Old Trafford
Muda: Saa 4:00 Usiku
Mfumo: Manchester United 4-4-1-1
Chelsea FC 4-4-1-1
Vikosi: Manchester United: De Gea, Jones, Ferdinand,
Vidic, Evra,
Valencia, Carrick, Giggs, Cleverley, Welbeck, Van Persie.
Chelsea:
Cech, Ivanovic, Terry, Cahill, Cole, Hazard, Lampard,
Ramires, Mata, Oscar,
Lukaku.
Mwamuzi: Martin Atkinson
Fuatana
nasi baadaye upate kila kitakachotea wakati wa mchezo huo
0 comments