Open top menu
Jumanne, 20 Agosti 2013

 Yohan Cabaye akiwa kazini

BAADA ya kuangukia pua katika mchezo wa kwanza wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Arsenal imetenga kitita cha pauni 10 milioni (zaidi ya 22 bilioni) kusana saini ya kiungo wa Newcastle, Yohan Cabaye.

Arsenal ambayo inamwania Luis Suarez wa Liverpool, ilianza vibaya msimu huu baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-1 kutoka kwa Aston Villa hali ambayo imeibua mjadala mkubwa kwa mashabiki wa klabu hiyo ambao wapo waliomtaka kocha wake Arsene Wenger kuachia ngazi.

Cabaye,27, alisafiri na timu yake hadi Manchester kuivaa Manchester City lakini hakucheza mchezo huo ambao waliambulia kipigo cha mabao 4-0, lakini alirudi nyumbani akionyesha kuwa hayupo tayari kiakili kuichezea timu hiyo kwa sasa.

 "Sitaki kuiamini ofa ya Arsenal," alisema Kocha wa Nerwcastle, Alan Pardew kuhusu ofa ya Arsenal.

Cabaye ambaye ameichezea Newcastle michezo 73 hadi sasa na kuifungia mabao 11 anatakiwa Arsenal kwa lengo la kuimarisha sehemu yao ya kiungo baada ya wachezaji wake kuwa majeruhi kama Mikel Arteta na Abou Diaby.

Newcastle hawana mpango wa kumuuza Cabaye, lakini hawanashindwa kuamia kwa haraka ili wasije yakawakuta kama yaliyoptokea kwa mshambuliaji wao, Andy Carroll mwaka 2011 ambaye walidai kuwa hawezi kuuzwa kwa dau lolote lile lakini mwisho wake walimuuza kwa Liverpool kwa ada ya uhamisho wa pauni 35 milioni.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments