Open top menu
Jumamosi, 24 Agosti 2013



MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu Tanzania Bara, Yanga imeanza vizuri mzunguko wa kwanza wa ligi hiyo baada ya kuitandika bila huruma timu ya Ashanti United mabao 5-1 katika mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

Wakati Yanga wakiikaribisha Ashanti kwa kipigo cha mbwa mwjizi mahasimu wao Simba wamepanwa mbavu mjini kwenye Uwanja wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora na Rhino Rangers baada ya kutoka sare ya mabao 2-2.

Mabao ya Yanga katika mchezo huo yalifungwa na Jerry Tegete dakika ya 11 na 47, Simon Msuva dakika ya 58, Haruna Niyonzima dakika ya 73 na Nizar Khalfan dakika ya 90 wakati bao la Ashanti lilifungwa na Abdallah Juma dakika ya 87 ya mchezo huo.

Kwa matokeo hayo Yanga inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi tatu na mabao matanonya kufungwa huku wakifungwa bao ikiwa ni mwanzo mzuri wa kutetea ubingwa wao.

Michezo mingine ya ligi hiyo, Ruvu Shooting waliibuka na ushindi mnono dhidi ya Prisons ya Mbeya wa mabao 3-0 katika mchezo uliochezwa kwenye uwanja wa Mabatini Mlandizi.

Mtibwa ambao walikuwa wenyeji wa Azam FC katika uwanja wa Manungu nje kidogo ya Morogoro walishindwa kuutumia vizuri uwanja wao wa nyumbani baada ya kulazimishwa sare ya mabao 1-1 na Wanarambaramba.

Coastal Union wameanza kwa kishindao ligi hiyo baada ya kushinda mchezo wake wa ugenini mjini Arusha kwa kuitandika JKT Oljoro mabao 2-0 mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Kumbukumbu za Shekh Amri Abeid.

Mchezo mwingine Maafande wa JKT Ruvu walianza vizuri ligi hiyo baada ya kuitandika wajeda wenzao Mgambo Shooting ya Tanga mabao 2-0 mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Mkwakwani mjini Tanga.

Mbeya wakiwa katika uwanja wa nyumbani waliibana mbavu Kagera Sugar na kuilazimisha sare ya bila kufungana katika mchezo mwao uliochezwa kwenye Uwanja wa Sokoine jijini Mbeya.

Matokeo ya mechi za leo
Yanga         5-1   Ashanti         
Mtibwa       1-1   Azam FC                     
JKT Oljoro 0-2   Coastal                        
Mgambo    0-2   JKT Ruvu                     
Rhino         2-2   Simba SC           
Mbeya City   0-0   Kagera             
Ruvu          3-0   Prisons          
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments