Open top menu
Jumatatu, 26 Agosti 2013


Kocha Mkuu wa Simba, Abdallah 'King' Kibaden



BAADA ya kutoka sare ya mabao 2-2 na Rhino Rangers ya Tabora, timu ya Simba imewasili mkoani Arusha kwa ajili ya mechi yao ya kesho dhidi ya JKT Oljoro, itakayopigwa kwenye Uwanja wa Sheikh Amri Abeid mjini humo.


Akizungumza na Nyumba ya Michezo na Burudani kwa njia ya simu jana, Kocha wa Simba, Abdallah 'King' Kibaden, alisema anashukuru wamefika salama na wapo tayari kwa ajili ya mechi hiyo.


Kibaden alisema anaamini muda waliotumia kufika Arusha unatosha kujipanga, ambapo wamewasili mjini humo juzi wakitokea Tabora moja kwa moja.


"Tutafanya vizuri katika mechi yetu hii licha ya kuanza vibaya, lakini hiyo ni moja ya matokeo ya mchezo wa soka, tumejiandaa vizuri na tumeanza kufanya mazoezi mepesi," alisema Kibadeni.


Alisema kupatikana kwa Hati za Uhamisho wa Kimataifa (ITC) za wachezaji kutoka Burundi Girbert Kaze na Amiss Tambwe kutasaidia kukiimarisha kikosi chake.


"Naamini kikosi changu kipo tayari kwa ajili ya mchezo huu dhidi ya Oljoro na ukizingatia wachezaji wangu wawili wamepata ITC, hivyo nina kila sababu ya kuibuka na ushindi katika mechi hiyo," aliongeza Kibadeni.


Kocha huyo wa zamani wa Kagera Sugar, alisema wameona upungufu uliojitokeza katika mchezo wao uliopita dhidi ya Rhino na kwamba wameshaufanyia kazi hususani suala la kipa wao, Abel Dhaira la kufungwa mabao yanayofanana.


Aliwataka mashabiki wa Simba wa jijini humo kujitokeza kwa wingi kuipa sapoti timu yao na wasikatishwe tamaa na matokeo ya sare waliyoyapata ugenini na kwamba ugenini kunakuwa na mambo mengi.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments