Tasnia ya ngumi nchini Tanzania jana iliingia aibu
mbele ya bondia mkongwe Francois Botha kutoka Marekani, baada ya bondia Mada
Maugo kutoka kupanda jukwaani kupambana na Fransic Mashali kwa zaidi ya nusu
saa.
Maugo aligoma kupanda ulingoni kwa madai kuwa
hajalipwa fedha zake kwa ajili ya mpambano huo wa raundi 10 wa kuwania mkanda
wa Afrika wa uzito wa feather dhidi ya Mashali.
Pambano hilo ambalo lilikuwa la utangulizi kabla ya
lile ya Fransic Cheka wa Tanzania na William wa Marekani, lilisubiri kwa muda
kutokana na kisanga hicho hadi pale bondia wa zamani wa uzito wa juu, Botha
kuingilia kati na kumwomba Maugo apande ulingoni na atamlipa yeye fedha zake.
Endelea kubaki ndani ya nyumba ili uendelee kupata
kinachojiri huko Diamond
0 comments