Pamoja na bondia Mada Maugo kugoma kupanda ulingoni
kwa muda lakini hakuepuka kipigo kutoka kwa mpinzani wake, Thomas Mashali baada
ya kutwangwa kwa pointi.
Mpambano huo ambao ilikuwa wa raundi 10 kuwania
mkanda wa Afrika wa uzito wa feather
ulikuwa na ushindani katika raundi zote lakini hadi kufika mwisho wa mpambano
huo, Mashali ameibuka kidedea kwa pointi.
Mashali amekabidhiwa mkanda na bondia wa zamani wa
uzito wa juu wa Marekani, Francois Botha hivyo kutawazwa rasmi kuwa bingwa wa
mkanda huo.
Usitoke
nyumbani endelea kupata kinachojili katika mapambano kati ya Francis Cheka na
William kutoka Marekani.
0 comments