Klabu ya Chelsea imemaliza ubishi baada ya kumsajili mshambualiaji mkongwe wa Cameroon, Samuel Eto'o kutoka katika klabu ya Urusi ya Anzhi Makhachkala.
Eto’o mwenye umri wa miaka 32 amesaini mkataba wa
mwaka mmoja kuitumikia klabu hiyo yenye maskani yake kwenye Uwanja wa Stanford Bridge
ikiwa ni mchezaji wa pili wa Anzhi Makhachkala kutua katika kikosi cha Jose Mourinho baada ya
kumsanisha Mbrazil Willian.
"Najisikia kuwa hapa lakini maamuzi haya
yametokea kwa kuwa nataka kucheza soka," alisema Eto'o alipohojiwa na
tovuti ya Chelsea.
"Yalikuwa ni maamuzi magumu sana kutua Chelsea.
Nimejua uwezo wa kisoka wa Chelsea na nimekuwa na furaha na Jose Mourinho kabla
ya kutua hapa, hivyo bahati ilipotokea nimejisikia vizuri kuifanyia kazi.”
0 comments