Open top menu
Jumatano, 21 Agosti 2013



KLABU ya soka ya Yanga, leo imewasilisha rasmi pingamizi juu ya adhabu aliyopewa winga wao, Mrisho Ngassa na kusisitiza ni lazima watani zao wa jadi, Simba waadhibiwe kwa kumsainisha mchezaji huyo akiwa katika mkataba na Azam FC.

Ngassa amefungiwa kucheza mechi sita na Kamati ya Katiba, Sheria na Hadhi za Wachezaji na kutakiwa kurejesha fedha za usajili alizopewa na klabu ya Simba Sh. 30 milioni na fidia ya asilimia 50 ya kiasi hicho alichopewa baada ya kusaini mkataba wakati akitokea Azam kwa mkopo.

Winga huyo aliyeruhusiwa kuichezea Yanga msimu ujao, alianza kuitumikia adhabu hiyo katika mechi iliyopita ya Ngao ya Jamii dhidi ya Azam.

Katibu Mkuu wa Yanga, Lawrance Mwalusako, aliiambia blog ya Nyumba ya Michezo na Burudani wameshalifanyia kazi suala hilo na kuamua leo au kesho watawasilisha rasmi pingamizi hilo.

"Tunawasilisha pingamizi kwa kamati ya rufaa kupinga uamuzi wa kamati ya Mgongolwa (Alex) kumpa Ngassa adhabu hiyo wakati tulikuwa sahihi kumsajili na tulifuata taratibu zote zinazotakiwa," alisema Mwalusako na kuongeza;

"Sisi tulimsajili Ngassa akiwa huru, lakini wenzetu (Simba) waliingia makubaliano naye akiwa ndani ya mkataba uliobaki miezi tisa kumalizika, tunashangaa hawajafungiwa."

Alisema kwa kanuni za usajili zinasema klabu inapaswa kufanya mazungumzo na mchezaji akibakisha miezi sita kabla ya mkataba kumalizika na ndicho walichofanya wao, sasa wanashangaa kupewa adhabu.

Alipoulizwa kuhusu Ngassa kuchukua fedha Simba na kusaini kwao, alisema suala hilo ni binafsi na ilipaswa Simba, Yanga na mchezaji husika kulijadili, lakini lilipelekwa sehemu ambayo si sahihi kujadiliwa.

Mwalusako alisema kutokana na hilo, ndiyo maana hata barua waliyoipata kutoka kwa kamati hiyo inayoelezea adhabu ya Ngasa haijawekwa wazi ni kifungu kipi kimetumika kumuadhibu mchezaji huyo.

Katibu huyo alisema mchezaji huyo ameonewa kwani kama zingefuatwa kanuni hata Simba ingelazimika kukumbwa na rungu hilo, na alisisitiza wapo tayari kukaa meza moja na watani zao kujadili suala hilo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments