Open top menu
Jumanne, 20 Agosti 2013


Mshambuliaji wa Manchester City, Sergio Aguero akifunga bao la pili.

KOCHA mpya wa klabu ya Manchester City, Manuel Pellegrini ameanza vizuri kibarua chake baada ya kuitandika Newcastle mabao 4-0 katika mchezo wake wa kwanza wa Ligi Kuu ya England.

Kwa ushindi huo Manchester City ndiyo inayoshikiria usukani wa ligi hiyo wakiwa na poindi tatu na mabao manne ya kushinda wakifuatiwa na Mahasimu wao watoto wa Moyes (David), Manchester United wenye pointi sawa lakini wao wameruhusu bao moja la kufungwa huku wakishinda manne.

Kikosi cha Pellegrini ambacho kilikuwa katika uwanja wa nyumbani wa Etihad, kilianza kuwainua mashabiki wake dakika ya sita ya mchezo huo kwa bao safi lililofungwa na kiungo wake, David Silva akimalizia pasi nzuri kutoka kwa mshambuliaji mwenye nguvu wa klabu hiyo, Edin Dzeko.

Sergio Aguero akishindilia msumali wa pili kwa Newcastle dakika ya 22 baada ya kufanya shambulio la ghafla na kumtoka beki wa timu hiyo na kuachia shuti ambalo lilijaa moja kwa moja wavuni na kumshinda kipa, Tim Krul na kujaa wavuni.

Newcastle ambao walimaliza mchezo huo wakiwa 10 baada ya Steven Taylor kutolewa kwa kadi nyekundu baada ya kumchezea vibaya Aguero, walijikuta wakiongezwa bao la tatu dakika ya 50 lililofungwa na Yaya Toure kwa faulo ya moja kwa moja iliyojaa wavumi kabla ya Samir Nasri kufunga pazia ya mabao kwa timu yake dakika ya 75.

Man City walionekana kuwa tishio kwa wapinzani wao dakika zote za mchezo kutokana soka safi waliolionyesha, huku wachezaji wake wapya waliotua klabuni hapo msimu huu, Fernandinho na Jesus Navas wakitakata katika eneo la kiungo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments