MCHEZA tenisi namba tatu kwa ubora kwa wanawake duniani,
Maria Sharapova amejiondoa katika michuano ya U.S. Open 2013 inayotarajiwa kuanza Jumatatu
ijayo jijini New York, Marekani.
Sharapova amefikia uamuzi huo kwa lengo la kujipa
muda ili auguze majeraha yake ya bega lake la kulia, nyota huyo hakuonekana
uwanjani kwa muda mrefu toka alipotolewa katika raundi ya pili katika michuano
ya Wimbledon mwezi Juni mwaka huu.
Mrembo huyo ambaye amecheza mechi moja ya mashindano
toka aumie, pamoja na kuonekana kurudi uwanjani wiki iliyopita akiutuymia jina
jipya la "Maria Sugarpova," lakini hatashiriki mashindano hayo
makubwa katika tenisi hadi awe fiti zaidi.
0 comments