Jamal Malinzi mgombea wa Urais wa TFF
Usaili kwa wanaoomba kuteuliwa kuwa wagombea uongozi
katika uchaguzi wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) na ule wa Bodi
wa Ligi Kuu (TPL Board) unaanza kesho (Agosti 30 mwaka huu).
Kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa na Kamati ya
Uchaguzi ya TFF, Agosti 30 mwaka huu ni usaili kwa waombaji uongozi wote katika
Bodi ya Ligi Kuu pamoja na waombaji uongozi wa TFF kwa kanda namba 11 (Morogoro
na Pwani), kanda namba 12 (Kilimanjaro na Tanga) na kanda namba 13 (Dar es
Salaam).
Agosti 31 mwaka huu ni kanda namba sita (Rukwa na
Katavi), kanda namba saba (Mbeya na Iringa), kanda namba nane (Njombe na
Ruvuma), kanda namba tisa (Lindi na Mtwara) na kanda namba kumi (Dodoma na
Singida).
Usaili kwa kanda namba moja (Geita na Kagera), kanda
namba mbili (Mara na Mwanza), kanda namba tatu (Simiyu na Shinyanga), kanda
namba nne (Arusha na Manyara) kanda namba tano (Kigoma na Tabora), na nafasi za
Rais na Makamu wa Rais wa TFF utafanyika Septemba Mosi mwaka huu.
Waombaji wote wamepangiwa muda wao wa usaili. Kwa
mujibu wa ratiba usaili ufanyika kuanzia saa 3 kamili asubuhi hadi saa 2 usiku.
Wasailiwa wote wanatakiwa kuzingatia muda waliopangiwa.
0 comments