Klabu ya Yanga imewatoa hofu waliokuwa wachezaji wao
Shadrack Nsajigwa, ambaye kwa sasa ni kocha wa Lipuli ya Iringa na Stephano
Mwasika aliyesajiliwa Ruvu Shooting kwamba watawalipa fedha zao wanazowadai.
Mwalusako alisema wamepata taarifa zisizo rasmi
kwamba wachezaji hao wamewasilisha
malalamiko yao kwa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) wakida hawataki
kuwalipa, jambo ambalo si kweli.
"Tunafanya mawasiliano ya mara kwa mara na
wachezaji hao na mwingine anadai yupo mbali, hivyo mchakato wa kuwalipa fedha
zao upo kama kawaida ila kwa sasa tunaweka mambo sawa na tutawalipa siku si
nyingi," alisema.
Nsajigwa anaidai klabu yake hiyo ya zamani Sh. 10 milioni,
huku Mwasika naye akidai milioni sita.
0 comments