MSHAMBULIAJI wa zamani wa klabu ya Manchester
United, Cristiano Ronaldo amewaambia viongozi wa timu hiyo, kuwa mipango
yake ni kuona siku moja anaichezea tena klabu hiyo.
Ronaldo ambaye aliuzwa na Manchester mwaka 2009 kwa
ada ya uhamisho iliyovunja rekodi ya pauni 80 milioni kwa Real Madrid,
amekuwa akihusishwa na kutaka kuihama klabu hiyo na kurudi tena Old Trafford.
Leo mshambuliaji huyo raia wa Ureno amevunja ukimya
baada ya kuwaambia Manchester United kuwa lazima atarudi kuichezea tena timu
hiyo na hata kama haitakuwa katika kipindi hiki cha usajili basi itakuwa
mwakani katika kipindi cha usajili cha majira ya joto.
Ronaldo ambaye mkataba wake na klabu ya Madrid
unatarajiwa kumalizika 2015 lakini ni ngumu kumaliza mkataba wake kwani kuna dalili nyingi
kuwa staa huyo amechoka maisha ya Bernabeu.
Manchester United ambao hawajazungumza kitu katika
mipango hiyo lakini wanaonekana wanajiandaa kumpokea mshambuliaji huyo kwani
tayari jezi namba saba ambayo msimu uliopita alikuwa akivaliwa na Antonio Valencia
amepokonywa na kuachwa ikiwa haina mtu.
Ronaldo alipokuwa Manchester United alikuwa akivaa
jezi namba saba hivyo wameshamuandalia mazingira ya kumrudishia jezi yake pindi
atakaporejea Old Trafford.
0 comments