IKIWA yamebaki masaa 48 kabla ya kufungwa kwa dirisha na usajili wa Ligi Kuu ya England, klabu ya Manchester United imekubali kuzungumza na Chelsea ili kumwachia mshambuliaji wao, Wayne Rooney kwa kubadilishana na Juan Mata.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho aliekeza nguvu zake
kwa Rooney baada ya kuwakosa washambuliaji aliokuwa anawawinda, Radamel Falcao,
Edinson Cavani na Robert Lewandowski lakini Kocha wake, David Moyes alisisitiza
kuwa nyota huyo yupo kwenye mipango yake na hawezi kuuzwa.
Baada ya kuwa na presha kubwa kutoka kwa Chelsea
inaonekana Man Utd wamelegeza kamba na kufungua milango ya mashambuliaji huyo
wa England kuondoka katika Uwanja wa Olkd Trafford.
United ambao walipanga kumwachia Rooney kwa pauni
milioni 40 (zaidi ya Sh 88 bilioni) lakini Chelsea walifika dau ya pauni 30
milioni (Sh 66 bilioni), hivyo sasa mpango huo unaweza kukamilika kama wakimtoa
fedha hizo pamoja na Mata.
Pande hizo mbili kwa pamoja zipo katika makubaliano
ya kubadilishana wachezaji hao lakini Chelsea kuna uwezekano wa kumuongeza na David
Luiz katika mpango huo ili iweze kuwashawishi United kumwachia Rooney kwa
urahisi zaidi.
"Wayne (Rooney) anaigiza kwa kufanya mazoezi
bila kinyongo na wenzake katika uwanja wa Carrington lakini hakuna siri kuwa
mipango yake ni kuondoka," alisema chanzo cha habari kutoka ndani ya Man United.
0 comments