Open top menu
Jumatatu, 26 Agosti 2013


Kikosi cha wachezaji wa Yanga


HATIMAYE uongozi wa Yanga umefanikiwa kuwalipa sh. milioni 50 kati ya milioni 100, wachezaji wake ikiwa ni sehemu ya ahadi yao ya kutwaa ubingwa msimu uliopita.


Mara baada ya kumalizika kwa Ligi Kuu msimu uliopita, na Yanga kutwaa ubingwa huo, uongozi uliwaahidi sh. milioni 100, ikiwa ni motisha kwa ajili ya kutwaa ubingwa huo uliokuwa ukitetewa na Simba, ambao walimaliza wakiwa nafasi ya tatu.


Mmoja wa wachezaji wa Yanga, ambaye hakutaka kuandikwa jina lake gazetini, aliiambia Nyumba ya Michezo na Burudani Dar es Salaam jana kuwa uongozi wao umefanikiwa kuwalipa milioni 50, huku ukiwaahidi kuwamalizia milioni 50 nyingine ndani ya wiki hii.


"Sisi tulikuwa tunaudai uongozi wetu milioni 100, kwani walituahidi, na wameamua kutulipa nusu, na iliyobaki wamesema watatumalizia ndani ya wiki hii," alisema mchezaji huyo nyota wa kikosi hicho.


Aidha nyota huyo alisema, fedha hizo zilikumbushwa na nahodha wao, Nadr Haroub 'Cannavaro' Jumamosi iliyopita kabla ya kwendwa uwanjani katika mechi yao na Ashanti, ambapo Yanga ilishinda mabao 5-1.


Mchezaji huyo aliongeza kuwa kwa sasa wanaendelea na kambi makao makuu ya klabu hiyo kwa ajili ya maandalizi ya mchezo wa kesho dhidi ya Coastal Union utakaipigwa katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.


Hata hivyo viongozi wa Yanga walishindwa kupatikana kuthibitisha kama taarifa hizo, lakini simu ya mkononi ya Makamu Mwenyekiti, Clemence Sanga na Katibu wake, Laurence Mwalusako bado hazina majibu.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments