Open top menu
Ijumaa, 6 Septemba 2013


Bondia wa Tanzania, Francis Cheka ambaye alikuwa  bingwa wa IBF katika bara la Afrika uzito wa kati (Super Middleweight) ameingia kwenye orodha ya mabingwa wa dunia iliyotolewa na Shirikisho la Ngumi za Kulipwa la Afrika IBF.

Cheka ameingia katika rekodi hiyo baada ya kumtwanga bondia kutoka Marekani, Phil William na kutawazwa kuwa bingwa wa dunia anayetambuliwa na Shirikisho la Ngumi la Dunia (WBF).

Ushindi wa Cheka sio tu kwa Tanzania bali na kwa bara la Afrika na dunia yote kwa ujumla. Cheka ameungana na mabingwa wengine wa dunia wa uziro wa kati (Super Middleweight) wanaotambuliwa na vyama na mashirikisho kadhaa.

Orodha hiyo ya mabingwa na mataji yao kwenye mabano ni Carl Froch wa Uingereza (IBF), Andre Ward wa Marekani (WBC), Andre Ward wa Marekani (WBA), Robert Stieglitz wa Ujerumani (WBO) na  Thomas Oosthuizen wa Afrika ya Kusini (IBO).

Ushindi wa Cheka umeifanya Afrika kuwa na mabondia wawiliu waliongia kwenye orodha hiyo kwani awali alikuwa Thomas Oosthuizen kutoka Afrika ya Kusini.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments