Open top menu
Ijumaa, 13 Septemba 2013


MJINI Magharibi imepata tiketi ya kucheza fainali ya michuano ya Copa Coca-Cola kwa vijana wenye umri chini ya miaka 15 upande wa wavulana baada ya kuing’oa Temeke kwenye nusu fainali iliyochezwa leo (Septemba 13 mwaka huu) asubuhi Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume, jijini Dar es Salaam.

Ushindi wa mabao 2-0 yaliyofungwa dakika za 30 na 63 kupitia Juma Ali Yusuf ndiyo yaliyoipa Mjini Magharibi tiketi ya kucheza fainali itakayofanyika kesho (Septemba 14 mwaka huu) Uwanja wa Kumbukumbu ya Karume kuanzia saa 9 alasiri.

Mjini Magharibi itacheza fainali hiyo na mshindi wa nusu fainali ya pili inachezwa leo jioni kwenye uwanja huo huo kati ya mabingwa watetezi Morogoro na Ilala.

Kwa upande wa wasichana Ilala imetinga fainali baada ya kuifunga Kinondoni mabao 2-0 katika nusu fainali ya kwanza. Mabao ya washindi yalifungwa dakika ya 27 na Fatuma Bahau wakati Happiness Lazoni alifunga la pili dakika ya 39.

Nusu fainali ya pili kwa wasichana itakuwa kati ya Mwanza na Mbeya.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments