Open top menu
Jumapili, 15 Septemba 2013


Bondia Floyd Mayweather akishangilia baada ya kutwaa ubingwa dhidi ya mpinzani wake 
BONDIA Floyd Mayweather wa Marekani ameendeleza rekodi yake ya kutoshindwa pambano lolote hadi sasa baada ya kumtwanga kwa pointi poindia wa Mexico, Saul Alvarez katika mpambano uliofanyika Alfajiri ya leo huko jijini Las Vegas, Marekani.

Bingwa huyo wa uzito wa light-middle mwenye umri wa miaka 36, anashikilia mataji WBC na WBA, ameshacheza mapambano 45 na hajapoteza hata moja hadi sasa.
 Mayweather akimsukumia konde mpinzani wake katika mpambano huo

Katika mpambano huo wa raundi 12, Mayweather alipewa ushindi ma majaji wawili na mmoja akimpa sare. Maamuzi hayo yalikuwa 114-114, 116-112, 117-111.

Ushindi huo wa Mayweather amevunja mwiko wa Alvarez ambaye hakuwahi kupoteza mpambano wake katika mapambano 42 aliyopigana. Alvarez hili ni pambano lake la kwanza kupoteza, hivyo kwa sasa ana rekodi ya kucheza mapambano 43 na ameshinda 42 na kupoteza moja. 
 Alvarez akijibu mapigo ya Mayweather kwa kusukuma konde lililotua shavuni kwa bingwa huyo

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments