Open top menu
Alhamisi, 26 Septemba 2013


IDADI ya kadi zilizotolewa katika michezo saba iliyochezwa wiki iliyopita inaonyesha kuwa Ligi Kuu Tanzania Bara kuwa haina nidhamu.

Katika michezo saba iliyochezwa kwa kukutanisha timu 14 zinazoshiriki ligi hiyo jumla ya kadi 22 zimetolewa huku zote zikiwa za njano.

Pamoja na kadi hizo kuwa za njano lakini haitoshi kuoinyesha kuwa katika michezo hiyo madhambi mengi yametendeka kiasi cvha kuwafanya waamuzi kuwaonya wachezaji kwa kadi hizo za njano.

Katika ripoti hiyo ya wiki iliyotolewa na Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) inaonyesha kuwa jumla ya michezo saba imechezwa mwishoni mwa wiki iliyopita Septemba 21 na 22 katika viwanja saba.

Jumla mabao yaliyofungwa katika michezo hiyo ni 18 yamefgungwa katika michezo yote saba ikiwa na idadi hiyo ya kadi zilizotolewa na waamuzi.

Mbali na kadi hizo zilizotolewa katika michezo hiyop saba lakini hadi sasa toka ligi hiyo ianze jumla ya kadi 116 zimetolewa huku nyekundu zikiwa tano na kadi za njano 111.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments