Open top menu
Jumanne, 24 Septemba 2013


KOCHA wa zamani wa Chelsea, Roberto de Matteo amependekezwa kuwa chaguo la kwanza kuziba nafasi iliyoachwa na Paolo Di Canio kuiongoza klabu ya Sunderland.

Taarifa zinasema kuwa Mkurugenzi wake Black Cats amekuwa na mipango ya kumshawishi Di Matteo kujiunga na timu yake kuziba pengo la Di Canio na mazungumzo yao yanatarajia kuanza wakati wowote kuanzia sasa.

Kama De Matteo atakubaliana na Sunderland ataanza kazi mapema iwezekanavyo kabla ya mchezo wao dhidi ya Manchester United utakaochezwa Oktoba 5 mwaka huu.

Makocha wengine ambao wanawaniwa na Black Cats ni pamoja na Gus Poyet na Tony Pulis lakini hao ni cxhaguao la pili kama mambo yatakuwa magumu kwa Di Matteo ambaye ni chaguo la kwanza la uongozi wa klabu hiyo.

Di Matteo amekuwa nje ya uwanja wa uwanja toka Novemba mwaka jana baada ya kutimuliwa na klabu ya Chelsea baada ya kuipa ubingwa wa Ligi ya Mabingwa Ulaya na Komnbe la FA katika miezi nane aliyoitumikia klabu hiyo ya Stamford Bridge.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments