Open top menu
Jumatano, 23 Oktoba 2013

VINARA wa Ligi Kuu ya England, Arsenal wamejiweka njia katika michuano ya Ligi ya Mabingwa Ulaya (Uefa) baada ya leo usiku kukubali kichapo cha mabao 2-1 kutoka kwa Borussia Dortmund.

Kwa matokeo hayo Arsenal wamejiweka katika mazingira magumu kusonga mbele kwani wanakabiliwa na michezo migumu ambayo watakuwa ugenini.

Matokeo ya mchezo huo uliochezwa kwenye Uwanja wa Emirates, Arsenal ipo katika nafasi ya pili katika Kundi F, ikiwa na pointi sita sawa na kminara wa kundi hiyo, Dortmund lakini pia ipo sambamba na Napoli wanaoshika nafasi ya tatu katika kundi hilo wakiwa na tofauti ya mabao.

Arsenal ndiyo wanaonekana kuwa katika mazingira magumu kutokana na kuwa na michezo miwili ya ugenini dhidi ya Napoli na watakaporudiana na Dortmund kabla ya kumaliza na Marseille Emirates, ili waweze kusonga mbele wanatakiwa kushinda michezo hiyo.
Dortmund ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao la kuongoza katika mchezo huo kupitia kwa kiungo wake Henrikh Mkhitaryan dakika ya 16 lakini mshambuliaji wa Ufaransa, Olivier Giroud aliisawazishia Arsenal dakika ya 41.

Mashabiki wa Arsenal hawawezi kumsahau Robert Lewandowski kwani ndiye alilizamishwa jahazi la timu hiyo baada ya kukwamisha msumali wa mwisho dakika ya 87 kwa shuti kali akiunganisha krosi ya Kevin Grosskreutz.

Mabao mawili ya Fernando Torres yaliiwezesha timu yake ya Chelsea kupata ushindi wa ugenini dhidi ya Schalke 04 wa mabao 3-0 na kuwafanya kuongoza kundi E.

Torres alifungwa bao la kwanza akiunganisha kichwa krosi ya Branislav Ivanovic dakika ya 15 kabla ya kuongeza la pili dakika ya 69 na Eden Hazard alishindiliwa msumali wa mwisho.

Katika mchezo mwingine wa Kundi H, FC Barcelona walishindwa kutamba wakiwa ugenini baada ya kulazimishwa sare ya bao 1-1 dhidi ya AC Milan, wenyeji ndiyo walikuwa na kwanza kupata bao kupitia kwa Robinho wakati bao la kusawazisha lilifungwa na Lionel Messi.

Matokeo mengine ya michezo ya leo ni kama ifuatavyo

Marseille          1 - 2  Napoli
Celtic                2 - 1  Ajax
Austria Wien    0 - 3  Atltico Madrid
Steaua               1 - 1   Basel

FC Porto          0 - 1  Zenit
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments