Open top menu
Alhamisi, 31 Oktoba 2013

Polisi wakiwafuata mashabiki wa Simba ambao walikuwa wanang'oa viti



 


BAO la beki wa kulia wa Kagera Sugar, Salum Kanoni lilipoteza amani ndani ya Uwanja wa Taifa baada ya mashabiki wa Simba kuanza kung’oa viti hali iliyosababiosha Polisi walipue mabomu ya machozi kutuliza vurugu hizo.

Kagera ambao walikuwa nyuma kwa bao 1-0 lililofungwa na Asimi Tambwe katika kipindi cha kwanza, walipata bao la kusaweazisha kupitia kwa Kanoni kwa njia ya panalti baada ya Joseph Owino kumwangusha Daudi Jumanne katika eneo la hatari.

Kwa sare hiyo hali ya Simba imeendelea kuwa tyete kwani bado wamebaki katika nafasi ya nne wakiwa na pointi 21 nyuma ya Yanga yenye pointi 22 huku Azam na Mbeya City wakiwa juu kwa pointi 23 kila moja wakitofautiana mabao ya kufunga.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa katika dakika zote kwani timu hizo zilikuwa zikihitaji pointi tatu ili wajiweke sehemu nzuri kabla ya kumaliza mzunguko wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara.


Simba itamalizia mzunguko wa kwanza kwa kucheza na Ashanti United mchezo utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Jumamosi ya Novemba 2.




Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments