Open top menu
Jumapili, 20 Oktoba 2013


Mshambuliaji wa Yanga Hamis Kiiza akifunga bao la pili katika mchezo huo huku Haruna Shamte na kipa Abel Dhaira wakiwa wameduwaa

SIMBA imeonyesha kuwa bado ni wababe katika Ligi Kuu ya Tanzania Bara baada ya kulazimisha sare wakiwa nyuma ya mabao 3-0 dhidi ya wapinzani wao Yanga katika mchezo wa ligi hiyo uliochezwa leo kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Katika mchezo huo ambao ulihudhuriwa na mashabiki lukuki kiasi cha kuuzaja uwanja huo, Simba walijikuta wakienda vyumbani wakiwa tayari wamekubali kipigo cha mabao matatu huku wakiwaaacha Yanga wakitawala mchezo kwa kipindi chote cha kwanza.

Yanga ambao walianza mchezo huo kwa kasi walipata mabao yao kupitia kwa Mrisho Ngassa ambaye alitangaza kuchoma nyumba zake tano kama hatafunga bao katika mchezo huo au kutoa pasi ya bao, hivyo kwa bao hilo ameokoa nyumba zake.

Mabao mengine mawili ya Yanga yalifungwa na Mganda, Hamis Kiiza akimalizia kazi nzuri za Didier Kavumbagu ambaye alimtengenezea mabao yote mawili.

Mashabiki wa Yanga walijua tayari wamemaliza kazi kwaki timu yao ilikuwa ikicheza soka safi huku wakiwa mbele kwa mabao matatu, lakini kibao kiligeuka na wapinzani wao kurudi kwa kutawala kipindi cha pili na kusawazisha mabo yote mawili.
 Beki wa Simba, Joseph Owino akiwa makini kuhakikisha Mrisho Ngassa asilete madhara langoni mwao

Mabao ya Simba katika mchezo huo yalifungwa na Betrum Mombeki, Said Hamis kabla ya Gilbert Kaze kuwaahamsha mashabiki wa Simba ambao waliamini kuwa wamelala katika mchezo huo.

Simba: Abel Dhaira, Said Nassor, Haruna Shamte, Gilbert Kaze, Joseph Owino, Jonas Mkude, Ramadhani Singano, Abdulhalim Humud/Said Hamis, Betrum Mombeki, Amis Tambwe na Haruna Chanongo/Willium Lucian.

Yanga: Ali Mustafa, Mbuyu Twite, David Luhende, Nadir Haroub, Kelvin Yondani, Athuman Idd, Haruna Niyonzima, Frank Domayo, Didier Kavumbagu, Mrisho Ngassa na Hamis Kiiza/ Simon Msuva
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments