Open top menu
Ijumaa, 11 Oktoba 2013


KOCHA Msaidizi wa timu ya Simba, Jamhuri Kihwelo ‘Julio’ amekiri kuwa kikosi chake ni kibovu lakini kwa ubovu huo huo waliokuwa nao, mahasimu wao Yanga watapokea kipigo katika mchezo wao wa kwanza wa Ligi Kuu Tanzania Bara si chini ya mabao matatu.

Simba ambayo inaongoza ligi hiyo ikiwa na pointi 15 baada ya kucheza michezo saba, inatarajia kuivaa Yanga katika mchezo wa raundi ya kwanza utakaochezwa Oktoba 20, 2013 kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Akizungumza na Nyumba ya Michezo na Burudani, Julio alisema kuwa watu wanasema kuwa Simba ni mbivu, wao wanakubali maneno hayo lakini timu hiyo inayoitwa mbovu ndiyo inayoongoza ligi na katika mchezo wao na Yanga wataibuka na ushindi mnono si chini ya mabao matatu.

Julio alisema hana wasiwasi na kikosi chake katika michezo inayoendelea ya ligi hiyo na anaamini kuwa katika mchezo wao na Yanga wataibuka na ushindi na kuendelea kukaa kileleni mwa ligi hiyo.

Kocha huyo aliyejaliwa kuwa na maneno mengi alisema kuwa katika kikosi chao hawana matatizo yoyote na wachezaji wao na taarifa zinzaotolewa zina malengo ya kuibua migogoro isiyokuwa na sababu.

“Simba haina ugomvi wowote kati ya wachezaji na makocha. Kinachoandikwa ni uzushi mtupu na kuthibitisha hilo tutaendeleza wimbi la ushindi na kutwaa ubingwa na timu hii ambayo kila mtu anaiona mbovu,” alisema Julio.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments