Open top menu
Jumanne, 29 Oktoba 2013

TIMU ya Yanga imeendeleza wimbi la ushindi wa mabao matatu baada ya leo kuitandika Mgambo Shooting mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Tanzania bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Huu ni ushindi wa pili mfululizo kwa Yanga kushinda mabao matatu dhidi ya Rhino Rangers na leo Mgambo, huku ikishinda tatu dhidi ya Simba lakini wakafanikiwa kusawazisha.

Yanga ambao walikuwa uwanjani bila ya nyota wake, Haruna Niyonzima, walipata bao la kwanz kupitia kwa beki wake kiraka, Mbuyu Twite dakika ya 32 kwa shuti kali ya faulo kufanya timu yake kwenda mapumziko wakiwa mbele. 

Dakika 52 Yanga waliongeza bao la pili kwa mkwaju wa penalti kupitia kwa Hamis Kiiza na kufunga bao lake na nane na kuwa sawa na kinara wa mabao Amisi Tambwe wa Simba, baada ya beki wa kipa wa Mgambo, Godson Mmasa kumwangusha mshambuliaji wa Yanga, Didier Kavumbagu.

Kavumbagu alishindilia msumali wa tatu kwa Mgambo kwa shuti kali lililomshinda kipa Mmasa na kutinga wavuni na kufanya Yanga kupata ushindi huo wa mabao matatu kwa mechi mbili mfululizo. 

Kwa matokeo hayo Yanga wamepanda hadi nafasi ya tatu na kuiacha Simba nafasi ya nne baada ya kufikisha pointi 22 wakiwa nyuma ya Mbeya City na Azam ambao wote wanapointi 23 huku wakitofautiana mabao ya kufunga na kufungwa.

Mbeya City nao wameitandika ndugu zao wa Prisons kwa mabao 2-0, shukrani kwa mabao ya Peter Mapunda dakika ya 67 na Deogratius Julius dakika ya 79.

Katika mchezo mwingine leo Rhino Rangers waliutumia vizuri uwanja wa nyumbani baada ya kuibuka na ushindi wa 1-0 dhidi ya JKT Ruvu, mfungaji akiwa Abbas Mohamed dakika ya 71.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments