Open top menu
Jumatano, 23 Oktoba 2013

KLABU ya Yanga jana iliwaliwaza mashabiki wake baada ya kuinyuka Rhino Rangers mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu Bara uliochezwa kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.

Mashabiki wa Yanga ambao waliondoka na simanzi katika mchezo wa watani wa jadi Simba mwishoni mwa wiki iliyopita baada ya kukubali sare ya mabao 3-3, baada ya leo kurudisha mabao hayo matatu.

Bao la kwanza la Yanga lilifungwa na Hamis Kiiza dakika ya 12 baada yua kumalizia kazi nzuri ya Simon Msuva ambaye aliwatoka mabeki na kupiga krosi safi na kufanya timu hizo zinaenda mapumziko Yanga wakiwa mbele kwa bao hilo moja.

Kazi nzuri ya Mrisho Ngassa ilizaa bao la pili baada ya pasi yake kumfikia Frank Domayo ambaye hakufanya ajizi na kukwamisha bao wavuni kwa shuti kali lilomshinda kipa wa Rhino, Mahamud Othman.

Pamoja na Kiiza kukosa mabao mengi lakini alijirekebisha na kukwamisha wavuni bao la tatu akimalizia kazi nzuri ya Ngassa ambaye alikuwa nyota wa mchezo huo.

Kwa matokeo hayo Yanga imefikisha pointi 19 wakati watani wao Simba wamefikiwa pointi 20.

Simba ambao walikuwa ugenini kwenye Uwanja wa Mkwakwani wakikabiliana na Coastal Union walishindwa kutamba ugenini baada ya kulazimishwa suluhu.

Yanga: Deogratius Munishi, Juma Abdul, David Luhende/Oscar Joshua, Kelivin Yondani, Mbuyu Twite, Rajab Zahir, Simon Msuva/ Nizar Khalfan, Frank Domayo, Haruna Niyonzima, Hamis Kiiza na Mrisho Ngassa.

Rhino Rangers: Mahamud Othman, Ali Mwanyiro, Hussein Abdallah, Julius Masonga, Ladslaus Mbogo, Stanslaus Mwakitos, Shija Mbogo, Oman Ndely/ Msafir Hamis, Victor Hangaya/Kamana Salum, Saad Kipanga na Nurdin Bakary.



Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments