Open top menu
Jumatatu, 21 Oktoba 2013


MABINGWA mara nne wa Afrika, TP Mazembe imefanikiwa kutinga kwenye hatua ya fainali bila ya kuwa na nyota wake watatu wa Zambia, baada ya kuinyuka CS Sfaxien ya Tunisia bao 1-0 mchezo uliochezwa jijini Lubumbashi jana.

Mazembe wamefanikiwa kutinga hatua hiyo baada ya kushinda kwa jumla ya mabao 3-1 baada ya kushinda mabao 2-1 katika mchezo wa kwanza uliochezwa jijini Tunis wiki mbili zilizopita.

Shukrani kwa bao la Kiungo wa DR Congo, Tresor Mputu na kuwahakikishia timu yake kucheza mchezo wa nfaiunali ambao utachezwa mwezi ujao.

Katika mchezo huo TP Mazembe waliwakosa wachezaji wake, Rainford Kalaba, Nathan Sinkala na Stoppila Sunzu ambao wamezuiliwa nchini kwao baada ya kugoma kuichezea timu yao ya Taifa ya Chipolopolo dhidi ya Brazil uliochezwa nchini China wiki iliyopita.

Wachezaji hao ambao waligoma kusafiri na timu hiyo kwa madai kuwa wanaumwa lakini serikali ya Zambia waliwanyang’anya hati za kusafiria za wachezaji hao hivyo wakashindwa kusafiri kwenda DR Congo kuitumikia klabu hiyo.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments