Open top menu
Ijumaa, 11 Oktoba 2013


MCHEZAJI wa kiungo cha kati wa timu ya taifa ya Ghana, Kevin-Prince Boateng atakosa mechi ya mkondo wa kwanza ya kujitafutia nafasi kucheza Fainali za Kombe la Dunia dhidi ya Misri, kutokana na jeraha la goti.

Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26, alipata jeraha hilo wakati wa mechi ya klabu yake ya Schalke ya Ujerumani kwenye mechi za Ligi ya Bundesliga.

Na baada ya kufanyiwa ukaguzi na madaktari, imegunduliwa kuwa Boateng lazima afanyiwe upasuaji kwenye goti lake la kushoto.

Kocha wa timu ya Black Stars, Kwesi Appiah, ameamua kutafuta mchezaji mwingine kuchukua nafasi ya Boateng.

Mechi za mkondo wa pili za kufuzu kwa kombe la dunia litakalochezwa nchini Brazil mwaka ujao, zitachezwa mjini Cairo, Misri tarehe 19 Novemba.

Hata hivyo, Ghana wameomba michuano hiyo kuhamishiwa kwingineko kwa sababu za usalama kufuatia hali ilivyo nchini Misri.



Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments