Open top menu
Jumatano, 30 Oktoba 2013

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Duniani (Fifa) limetoa majina ya wachezaji 23 watakaowania tuzo za mwanasoka Bora wa Dunia kwa mwaka 2013 ‘FIFA Ballon d’Or’.

Wachezaji hao 23 waliotangazwa watachujwa mwezi Desemba mwaka huu na kubaki wachezaji watatu ambao wataingia kwenye hatua ya mwisho ya fainali itakayofanyika Januari 13, 2014 jijini Zurich, Uswisi.

Hicho cha kutoa tuzo hiyo pia kutachaguliwa kikosi bora cha mwaka, kocha bora, mchezaji bora wa kike, beki bora, golikipa bora, kiungo na mshambuliaji bora wa dunia.

Majina ya wachezaji hao na nchi zao kwenye mabano ni Gareth Bale (Wales), Edinson Cavani (Uruguay), Radamel Falcao (Colombia), Eden Hazard (Ubelgiji), Zlatan Ibrahimović (Sweden), Andres Iniesta (Hispania), Philipp Lahm (Ujerumani), Robert Lewandowski (Poland), Lionel Messi (Argentina), Thomas Muller (Ujerumani), Manuel Neuer (Ujrumani), Neymar (Brazil) na Mesut Ozil (Ujerumani).

Wengine ni Andrea Pirlo (Italia), Franck Ribéry (Ufaransa), Arjen Robben (Uholanzi), Cristiano Ronaldo (Ureno), Bastian Schweinsteiger (Ujerumani), Luis Suarez (Uruguay), Thiago Silva (Brazil), Yaya Toure (Ivory Coast), Robin Van Persie (Netherlands) na Xavi (Hispania).

Kwa upande makocha waliotajwa katika orodha ya kuwania tuzo ya kocha bora wa dunia nchi zao na timu wanazofundisha kwenye mabano ni Carlo Ancelotti (Italia/Paris Saint-Germain FC/Real Madrid CF), Rafael Benítez (Hispania/Chelsea FC/SSC Napoli), Antonio Conte (Italia/Juventus) na Vicente Del Bosque (Hispania/Timu ya Taifa ya Hispania).


Wengine ni Sir Alex Ferguson (Scotland/Kocha wa zamani wa Manchester United), Jupp Heynckes (Germany/Kocha wa zamani wa FC Bayern München), Jurgen Klopp (Germany/Borussia Dortmund), Jose Mourinho (Ureno/Real Madrid CF/Chelsea FC), Luiz Felipe Scolari (Brazil/Timu ya Taifa ya Brazil), Arsene Wenger (Ufaransa/Arsenal FC).
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments