Open top menu
Jumapili, 27 Oktoba 2013

MCHEZAJI ghali wa dunia, Gareth Bale jana alishindwa kutamba katika El Clasico yake ya kwanza toka alipotua katika klabu ya Real Madrid walipovaana na Barcelona ambao waliibuka na ushindi wa mabao 2-1, mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa Camp Nou.

Bale ambaye alikuwa nje ya uwanja kwa muda akiwa anasumbuliwa matatizo ya mgongo, lakini jana alipangwa katika kikosi cha kwanza cha mchezo huo na Kocha wake, Carlo Ancelotti, lakini alishindwa kuonyesha kiwango kizuri na kuwaacha Barca watawale zaidi katika kipindi chote cha kwanza.

Ancelotti aliona mapungufu ya Bale na kulazimika kumtoa katika kipindi cha pili na nafasi yake kuchukuliwa na Kareem Benzema ambaye aliipa uhai timu yake lakini bado hawakuweza kutamba mbele ya Barca. 

Neymar ambaye naye ilikuwa Eli Clasico yake ya kwanza aling’ara katika mchezo huo na kuifungia timu ayke bao la kwanza dakika 19 wakati Sanchez aliongeza bao la pili akitumia uzembe wa kipwa wa Madrid, Diego Lopez baada ya kutoka mbele na kuliacha goli wazi.


Bao la Madrid lilifungwa na Jese Rodriguez katika dakika tatu za nyongeza na kuifanya timu yake kulala kwa mabao 2-1 katika mchezo huo.





Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments