Open top menu
Jumapili, 13 Oktoba 2013


MECHI ya Ligi Kuu ya Vodacom (VPL) kati ya wenyeji Simba na Tanzania Prisons kutoka Mbeya iliyochezwa jana (Oktoba 12 mwaka huu) Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam imeingiza sh. 60,521,000.

Simba iliibuka na ushindi wa bao 1-0 katika mechi hiyo namba 55 na kushuhudiwa na watazamaji 10,494 waliokata tiketi kwa viingilio vya sh. 5,000, sh. 8,000, sh. 15,000 na sh. 20,000.

Kila klabu ilipata mgawo wa sh. 14,191,002.55 wakati Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) iliyolipwa ni sh. 9,232,016.95.

Mgawo mwingine wa mapato hayo ni asilimia 15 ya uwanja sh. 7,215,763.96, tiketi sh. 3,183,890, gharama za mechi sh. 4,329,458.37, Kamati ya Ligi sh. 4,329,458.37, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) sh. 2,164,729.19 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) sh. 1,683,678.26.

Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments