Open top menu
Jumanne, 15 Oktoba 2013


MCHEZAJI soka wa Nigeria, Nosa Igiebor alijeruhiwa vibaya wakati timu yao iliposhambuliwa mjini Addis Ababa baada ya mchuano wao wa mchujo dhidi ya Ethiopia katika kutafuta nafasi ya kushirki kombe la dunia mwaka ujao nchini Brazil.

Mchezaji huyo ambaye huchezea timu ya Real Betis alihitaji matibabu ya dharura mkononi mwake baada ya dirisha la basi walimokuwa kuvunjwa wakati timu hiyo ilipokua inaondoka katika mji mkuu Addis Ababa. Alijeruhiwa kwa vioo.

Nigeria, ilishinda mabao mawili kwa moja na wameripoti tukio hilo kwa Fifa.

"Tunatumai kuwa Fifa itachukua hatua za kinidhamu," alisema Makamu Rais wa Shirikisho la Soka la Nigeria, Mike Umeh. "Ni jambo la aibu sana kwa tukio kama hili lilitokea baada ya mechi.”

Ben Alaiya, Afisa wa uhusiano mwema wa timu ya taifa ya Super Eagles alimuunga mkono Umeh katika kulaani tukio hilo.

Alaiya alisema kuwa mashabiki walishambulia basi iliyokuwa imewabeba wachezaji wa timu ya Nigeria kwa mawe ambayo yalivunja mojawapo ya dirisha la basi hivyo kulazimisha wachezaji kukimbilia usalama wao.

Walisema kuwa Igiebor hakubahatika kwani jiwe liligonga mkono wake na kusababisha damu kuvuja sana

Super Eagles wa Nigeria ndio wanaonekana kuwa katika nafasi nzuri ya kufuzu kucheza katika michuano ya kuwania kombe la dunia watakapocheza mechi ya marudiano mjini Calabar tarehe 16 Novemba.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments