Open top menu
Jumatano, 9 Oktoba 2013


Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akikabidhi jezi kwa Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Pool Tanzania (TAPA), Amos Kafyunga, pembeni kushoto ni nahodha wa timu ya Taifa ya Pool, Chaerles Venance na kulia ni Meneja wa timu hiyo, Nabil Hizza.

KAMPUNI ya Bia Tanzania (TBL) kupitia bia yake ya Safari Lager imetoa Sh 67 milioni kuidhamini timu ya Taifa ya Tanzania ya mchezo wa Pool katika ushiriki wake wa mashindano ya Afrika ya mchezo huo yatakayofanyika nchini Malawi.

Akizungumza na Nyumba ya Michezo na Burudani leo, Meneja wa bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo alisema fedha hizo walizotoa zitatumika katika kulipia gharama za usafiri, malazi na posho kwa kipindi chote timu itakapokuwa safarini.

Shelukindo alisema nia ya TBL kupitia Safari Lager kudhamini timu hiyo ni kuendleza mchezo wa Pool sambamba na kuibua vipaji vya vijana na kuwasaidia kiuchumi.

Meneja wa Bia ya Safari Lager, Oscar Shelukindo akizungumza na waandishi wa habari (hawapo pichani), pembeni yake kulia ni Katibu Mkuu wa Chama cha Mchezo wa Pool Tanzania (TAPA), Amos Kafyunga, kushoto ni nahodha wa timu ya Taifa ya Pool, Chaerles Venance na kulia mwisho ni Meneja wa timu hiyo, Nabil Hizza.
 
Kwa upande wake, Meneja wa timu hiyo, Nabil Hizza aliwataja wachezaji ambao wameingia kambini katika hoteli ya Picolo iliyopo Kawe, kuwa ni Mohamed Idd, Festo Yohana, Patrick Nyangusi, Omari Akida, Fred Steven, Geofrey Swai, Abdallah Hussein, Innocent Sami na nahodha wao Charles Venance.

Timu hiyo kabla ya kwenda kwenye mashindano hayo yatakayofanyika mwishoni mwa mwezi huu, inatarajia kucheza mechi ya kirafiki na timu ya taifa ya Kenya mchezo utakaochezwa Oktoba 12 mwaka huu jijini Arusha.


Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments