Open top menu
Alhamisi, 31 Oktoba 2013

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Gareth Bale baada ya kuchemsha katika mchezoi dhidi ya FC Barcelona jana alirudi katika kiwango cha hali ya juu na kuisaidia timu yake kuiangamiza Sevilla mabao 7-3 katika mchezo wa Ligi Kuu ya Hispania ‘La Liga’.

Katika mchezo huo Bale aliifungua Madrid mabao mawili huku akitoa pasi za mabao mawili kati ya matatu yaliyofungwa na nyota wa timu hiyo, Cristiano Ronaldo ambaye alikuwa mwiba wa Sevilla katika mchezo huo.

Mabao mengine mawili ya Madrid yalikwamishwa wavuni na Karim Benzema na kuhitimisha ushindi wa mabao hayo saba na kufanikiwa kujiliwaza na kipigo cha Barca.


Mabao ya kufutia machozi ya Sevilla yalifungwa na Ivan Rakitic aliyetupia mabao mawili na bao moja lilifungwa na Carlos Bacca wakati mchezaji wao, Mcameroon Stephane Mbia alitolewa nje kwa kadi nyekundu.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments