Open top menu
Jumatatu, 28 Oktoba 2013

DEREVA wa timu ya mbio za magari yaendayo kasi ya Formula One ‘Langalanga’ wa Redbull, Sebastiani Vettel amewadhihirishia mapenzi wa mashindano hayo kuwa hana mpinzani kwa sasa baada ya kutawazwa kuwa bingwa wa mbio hizo mwaka huu huku kukiwa bado mashindano hayo yajamalizika.

Vettel ametangazwa kuwa bingwa wa Langalanga 2013 jana usiku baada ya kushinda mbio zilizofanyika nchini India huku kukiwa badoi kumebakia na mashindano matatu ya mbio hizo.

Mjerumani huyo mwenye umri wa miaka 26 aliendesha gari lake bila matatizo yoyote kufanikisha ushindi wake wa mara ya sita mfululizo msimu huu na kujitokeza kuwa dereva wa nne katika historia ya mashindano haya kufanya hivyo.

Baada ya mbio hizo Vettel alisema, nashindwa hata kusimulia, nimevuka msitari wa kumaliza mbio nikapoteza kauli. Najitahidi kutafuta maneno lakini nashindwa. Ni msimu mzuri kwake, timu yake  ina furaha kubwa sana.

Ushindi huu ni wa sita mfululizo na wa kumi kwa ujumla wa msimu mzuri kwake ambao unaweza kumsogeza karibu na rekodi inayoshikiliwa na Schumacher aliyeshinda jumla ya mbio 13 katika msimu mmoja.

Licha ya uwezo wake wa kushinda hata hivyo, Vettel ameshindwa kuwa na mvuto katika ushindi wake. Mfano ni ushindi wake huko Ubelgigi, Uingereza, Canada na Singapore ambako alizomewa na kwenye medani ya India alisimulia na jinsi kuzomewa huko kulivyomuathiri.

Amesema kuwa nilizomewa ingawa sikufanya kosa lolote na hilo liliniudhi kiasi lakini majibu nimeyatoa kwa ushindi uwanjani.

Endapo Vettel atashinda mbio tatu zilizosalia huko Abu Dhabi, Marekani na Brazil atafikia pia ushindi wa mara tisa wa Albert ASCARI wa mwaka 1952 na 1953.


Hata hivyo mpango mpya wa utaratibu utakaoanza mwaka 2014 kuendelea mbele ukihusisha mfumo mpya wa Ingini za magari pamoja na mfumo wa kuwezesha ingini ziongezewe nguvu --yanaweza kuzidisha ushindani wa mbio hizi.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments