Open top menu
Jumatatu, 7 Oktoba 2013


Wachezaji wa West Ham United wakishangilia moja ya mabao yao katika mchezo wao dhdi ya Tottenham Hortspur jana usiku.

LIGI Kuu ya England jana iliendelea katika viwanja tofauti lakini michezo iliyokuwa gumzo ni kati ya West Ham United na Tottenham Hortspur, Arsenal dhidi ya West Brom huku Chelsea ikiwavaa Norwich City.

Katika michezo hiyo timu ya Tottenham walijikuta wakiangukia pua wakiwa nyumbani baada ya kukubali kichapo cha mabao 3-0 kutoka kwa West Ham United mchezo uliochezwa kwenye Uwanja wa White Hart Lane

Arsenal nao waliponea kwenye tundu la sindano kupoteza mchezo wao ambao walikuwa ugenini baada ya kutoka sare ya mabao 1-1 dhidi ya West Brom ambao walitangulia kupata bao na Arsenal kuchomoa kipindi cha pili.

Lakini kwa upande wa Chelsea wao walifanikiwa kuvuna pointi tatu baada ya kuinyuka Norwich mabao 3-1 katika mcheoz huo ambao ulikuwa na ushindani mkubwa.

Hakuna mtu aliyetarajia kwamba Tottenham wangechapwa namna hivyo hasa kwa kuzingatia kuwa ndiyo iliyovunja rekodi ya pesa nyingi za kuwanunua wachezaji wapya.

Mabao ya West Ham katika mchezo huo yalifungwa na Winston Reid dakika ya 66 na Ricardo Vaz Te akafunga bao la pili dakia sita baadae na Ravel Morrison ndiye aliyefunga bao la tatu.

Huo ni ushindi wa kwanza wa West Ham kwenye uwanja wa White Hart Lane tangu mwaka 1999 na ni ushindi wa kwanza wa ugenini tangu msimu huu kuanza. Katika mchezo mwingine Southamptom waibugiza Swansea 2-0.







Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments