Open top menu
Alhamisi, 10 Oktoba 2013


MALKIA wa Uingereza ameanzisha rasmi mbio za kupokezana rungu la michezo ya Jumuiya ya Madola itakayofanyika mjini Glasgow Scotland mwaka 2014.

Rungu hiyo ina risala aliyoiandika kwa mkono Malkia kwa Jumuiya ya Madola itakayosafirishwa katika mataifa na maeneo yote 70 yatakayoshiriki katika michezo hiyo katika kipindi cha siku 288 zijazo.

Rungu hilo litasafirishwa kwanza hadi Scotland mnamo siku ya Alhamisi kabla ya kuelekea India kwa kituo chake cha kwanza cha kimataifa Oktoba 11.

Safari ya rungu hilo itamalizika wakati wa sherehe za ufunguzi za michezo hiyo Julai 2014, ambapo Malkia ataisoma risala iliyomo ndani yake.

Katika sherehe za uzinduzi ziliofanyika katika kasri ya Malkia mjini London, Rais wa Shirikisho la michezo ya Jumuiya ya Madola, Prince Imran wa Malaysia, amesema mbio za rungu hilo lina ujumbe mzito wenye maana.

"Mbio za kupokezana rungu hilo zinawaunganisha raia billioni 2 wa Jumuiya ya Madola katika kusherehekea michezo, kabila tofauti na amani na kudumisha urafiki na uhusiano wetu" alisema Imran.

Baada ya hotuba Malkia alitumbukiza waraka wenye risala yake ndani ya rungu hilo na kisha kufungwa kwa safari yake ya kilometa 190,000 kupitia mabara ya Asia, Oceania, Afrika, Amerika za Kaskazini na Kusini na Caribbean.

Wa kwanza kukimbiza rungu hilo alikua Alan Wells, mwanariadha wa mbio fupi wa Scotland aliyeshinda medali ya dhahabu katika mbio za mita 100 za Olimpiki ya 1980 mjini Moscow.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments