Open top menu
Jumatatu, 21 Oktoba 2013




NAHODHA wa zamani wa England, Rio Ferdinand na Kocha wa timu hiyo, Roy Hodgson ameongezwa katika Tume iliyoundwa na Chama cha Soka cha England (FA) kwa lengo la kuboresha kikosi cha timu ya Taifa ya England, Three Lions kitakachoshiriki fainali za Kombe la Dunia 2014 nchini Brazil.

Ferdinand na Hodgson wameongezwa ikiwa siku moja baada ya Heather Rabbatts kuikosoa FA kwa kuchagua wajumbe wazungu pekee kuunda tume hiyo ambayo itakuwa na kazi ya kutoa mapendekezo ya kuiboresha gtimu hiyo kabla ya kushiriki fainali hizo.

Hodgson, 66, ndiye aliyeiwezesha timu ya England kutinga katika fainali hizo za 2014 zitakazofanyika nchini Brazil mwakani wakati Ferdinand, 34, aliichezea timu hiyo michezo 81 kabla ya kuamua kustaafu mwezi Mei mwaka huu.

Mwenyekiti wa FA, Greg Dyke alisema Ferdinand alikuwa katika mipango ya kujumuishwa katika tume hiyo kwani ana umuhimu mkubwa.

"Tumezungumza na Rio na klabu yake ya Manchester United kwa vipindi tofauti juu ya kumjumuisha katika tume hiyo kabla ya kutaja jina lake," alisema Dyke.

"Kwa sasa Ferdinand anaitumikia klabu ya Manchester United tulikuwa tunahitaji kupata uhakika kama ataweza kuhudhuria katika kamati hiuyo pindi atakapohitajika. Tumekubaliana kuwa ataweza kuifanya kazi hii tuliyompa."

Ferdinand na Hodgson wataungana na Makamo Mwenyekiti wa FA, Roger Burden, Kocha wa zamani wa England, Glenn Hoddle, beki wa zamani wa England, Danny Mills, Meneja wa Mwenyekiti wa FA, Howard Wilkinson, Ritchie Humphreys, Mweniekiti wa ligi, Greg Clarke mna Dario Gradi.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments