Open top menu
Jumatano, 9 Oktoba 2013


MSHAMBULIAJI wa kimataifa wa Cameroon, Samuel Eto’o amekubali kubadili maamuzi yake ya kustaafu kucheza soka la kimataifa baada ya kuomba na Rais wa nchi hiyo, Paul Biya.

Eto’o anayeichezea timu ya Chelsea kwa sasa, aliwatangazia wachezaji wenzake mwezi uliopita kuwa hataichezea tena timu hiyo lakini Rais Biya amemuomba nyota huyo kubadiliusha maamuzi yake na kuitumikia tena nchi yake.

Baada ya rais huyo kuzungumza na Eto'o, amekubali kuichezea Cameroon kwa mara nyingine na sasa atakwenda Ufaransa kujiunga na wachezaji wenzake kujiandaa na mchezo wao dhidi ya Tunisia utakaochezwa Jumapili ya Oktoba 13 kuwania kufufuzu fainali za Kombe la Dunia Brazil mwaka 2014.

“Unaweza kuwa na matatizo popote pale utakapokuwepo duniani, lakini cha muhimu kuangalia jinsi ya kuyamaliza,” alisema Eto’o. “Sasa nimeamua kurudi tena na nitajiunga na wachezaji wenzangu katika mchezo na Tunisia na kurudi kwangu kutakuwa na matokeo mazuri.”

Licha kuwepo ripoti za Eto’o kuacha kucheza soka, kocha wa timu ya Cameroon Volker Finke alimteua mshambuliaji huyo katika kikosi kitakachoivaa Tunisia.

Eto'o amekuwa na uhusiano tete na maafisa wa soka nchini Cameroon katika siku za nyuma ikiwemo hata kuongoza timu ya taifa kwenye mgomo uliosambaratisha mechi ya kirafiki dhidi ya Algeria.

Eto’o aliadhibiwa kwa kupigwa marufuku kucheza mechi 15 ingawa baada ya kukata rufaa alipunguziwa adhabu hadi mechi 8

Hata baada ya adhabu yake kumalizika alikataa kuichezea Cameroon kwa miezi kadhaa. Hii siyo mara ya kwanza kwa Rais Biya kuingilia kati na kumzuia mchezaji kujiuzulu kutoka katika majukumu ya kitaifa.
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments