Open top menu
Jumapili, 27 Oktoba 2013

HABARI zilizotufikia hivi punde mtandao huu, zinasema kuwa, Baba Mzazi wa msanii wa Filam nchini na Miss Tanzania wa mwaka 2006, Wema Sepetu, Balozi Issac Abraham  Sepetu, amefariki Dunia asubuhi ya leo katika Hospitali ya TMJ Mikocheni jijini Dar es Salaam, alikokuwa amelazwa.

Aidha imeelezwa kuwa, Balozi Sepetu alikuwa amelazwa katika hospital ya TMJ akitibiwa ugonjwa wa Kisukari na kiharusi uliokuwa ukimsumbua.

Hadi umauti unamkuta,Balozi Isaac Sepetu alikuwa ni Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Uwekezaji wa Vitega Uchumi Zanzibar.

Mtandao huu unaungana na waombolezaji wote wa Msiba huu na Mwenyezi Mungu, Aiweke Roho ya Marehemu Balozi Isaac Abraham Sepetu, Mahala Pema Peponi .

-Amen-


Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments