Open top menu
Jumapili, 27 Oktoba 2013

KIKOSI cha Arsene Wenger kimeendelea kujichimbia kileleni katika msimamo wa Ligi Kuu ya England, baada ya kushinda mchezo wake dhidi ya Crystal Palace mabao 2-0 uliochezwa jana.

Kwa ushindi huo Arsenal wamefikiwa pointi 22 wakifuatiwa na Liverpool wanaoshika nafasi ya pili wakiwa na pointi 20 nao baada ya kushinda mchezo wao jana.

Mashabiki wa Arsenal walisubiri hadi kipindi cha pili ndipo wainuke na kuanza kushangilia bao lao la kwanza kupitia kwa kiungo mshambuliaji, Mikel Arteta kwa njia ya penalti kabla ya Olivier Geroud kufunga kazi dakika chache kabla ya kipenga cha mwisho kulia.
Robin van Persie akiwa chini ya ulinzi wa wachezaji wa Stoke City
Katika mchezo mwingine Manchester United ilibuika na ushindi kwa mbinde dhidi ya Stoke City wakiwa nyumbani na kufanikiwa kushinda mchezo huo kwa mabao 3-2.

Katika mchezo huo ambao ulikuwa mkali na ushindani mkubwa, Stoke ndiyo walikuwa wa kwanza kupata bao lililofungwa na Peter Crouch kabla ya Robin van Persie kusawazisha lakini mkwaju wa faulo wa Marko Arnautovic uliomshinda kipa wa Manchester United, David da Gea na kujaa wavuni na kuwafanya wenyeji waende mapumziko wakiwa nyuma kwa mabao 2-1.

Mabao ya Wayne Rooney katika kipindi cha pili na Chicharito ambayo yote yalifungwa kwa kichwa ndiyo yaliyopeleka shangwe Old Trafford na kufanya Man Utd kuibuka na ushidni huo wa mabao 3-2.
Mshambuliaji wa Manchester United, Chicharito akifungao bao la tatu kwa kichwa 
Nao Liverpool jana walifanya mauaji baada ya kuikandamiza West Bromich mabao 4-1 huku Luis Suarez akionekana kurudi kwa kasi na kufunga hart-trick wakati bao linguine lilifungwa na Daniel Sturridge na bao la kufutia machozi la West Brom lilifungwa na James Morrison.

Matokeo mengine ya michezo iliyochezwa jana Everton ikichezea ugenini imeifunga Aston Villa mabao 2-0. Norwich imetoka suluhu na Cardiff City na Southampton ikaifunga Fulham mabao 2-0.


Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments