Open top menu
Jumanne, 15 Oktoba 2013


TIMU ya Taifa ya Zambia Chipolopolo ikiwa chini ya kocha wa mpito Patrice Beaumelle inashuka dimbani leo kukipiga dhidi ya mabingwa wa dunia mara tano Brazil kwenye mchezo wa kirafiki utakaopigwa kwenye Uwanja wa Birds Nest.

Mabingwa hao wa zamani wa Africa watakuwa bila ya mshambuliaji Rodger Kola, Collins Mbesuma, kiungo Mukuka Mulenga na beki Davies Nkausu ambao ni majeruhi.

Pia wachezaji Nathan Sinkala, Stopilla Sunzu, Rainford Kalaba wameshindwa kuripoti kwa wakati kwenye maandalizi ya mchezo huo.

Lakini kocha Beaumelle anaamini atachezesha kikosi imara na inawezekana akaamua kuwaanzisha wachezaji wanaocheza ligi ya nyumbani Bronson Chama, Kondwani Mtonga na Bruce Musakanya ambao watachanganywa na wazoefu Hichani Himonde, Kampamba Chintu na Joseph Musonda lakini pia inawezekana wakacheza Jimmy Chisenga au Emmanuel Mbola.

Nahodha Christopher Katongo, Noah Chivuta, Chisamba Lungu na Fwayo Tembo wapo kamili kuitumikia Zambia kwenye mchezo huo ambapo Jacob Mulenga kuongoza mashambulizi na James Chamanga huku Emmanuel Mayuka likiwa ni chaguo lingine.
Brazil kwa upande wao watakuwa bila ya kipa Julio Cesar, beki Thiago Silva na mshambuliaji Fred.
Felipe Luiz Scolari anatarajia kufanya mabadiliko kadhaa Diego Cavalieri atambadili Jefferson langoni wakati Daniel Alves, Dedé, David Luiz na Maxwell watatengeneza ukuta.

Lucas Leiva, Paulinho na Ramires wanatarajiwa kuanza kwenye kiungo huku Lucas, Alexandre Pato na Jo wakiwa kwenye ushambuliaji.

Hii ni mara ya kwanza kwa timu hizo kukutana
Tagged
Different Themes
Written by Templateify

Aenean quis feugiat elit. Quisque ultricies sollicitudin ante ut venenatis. Nulla dapibus placerat faucibus. Aenean quis leo non neque ultrices scelerisque. Nullam nec vulputate velit. Etiam fermentum turpis at magna tristique interdum.

0 comments